||

WOCHATA

WOCHATA

WOCHATA

WOCHATA

WOCHATA

WOCHATA

Tuesday, 30 September 2014

PSI NA TPSF KUWAWEZESHA WANAWAKE TANGA

Zikiwa zimebaki siku 14 tu kufanyika kwa ile Shughuli ya Wochata Jol inayosubiriwa kwa hamu na wakazi wa mkoa wa Tanga. PSI na TPSF wameahidi kuja kuwaelimisha Wanawake wa Tanga na kuwawezesha kupata fursa za kupata elimu ya Afya ya uzazi (PSI) na Ujasiriamali (TPSF).
PSI ni moja ya mashirika makubwa duniani yanayotoa huduma za afya hapa nchini. Ambapo TPSF wao ni taasisi ya sekta binafsi Tanzania.

Mashirika haya mawili yatatoa Wawakilishi kuja kuwaelemisha Wanawake wa Tanga katika Shughuli ya Wochata Jol itakayofanyika tarehe 14 Oktoba 2014, katika ukumbi wa Regal Naivera Tanga.



MIRIAM MIGOMBA: " PATAKUWA HAPATOSHI TAREHE 14 OKTOBA 2014"

Mwanadada Mc mahiri, Miriam Migomba amezungumzia tukio la wochata jol kuwa litaweka historia na kubadilisha maisha ya wanawake wa Tanga. Akiongea kwa njia ya simu na blogu hii amesema amejiandaa vya kutosha kuja kutoa somo kwa watakaoshiriki siku hiyo.

Mwanadada Miriam Migomba 

"Nachoweza kusema wanawake wenzangu wa Tanga, watambue kuwa kama hatuna desturi ya kukumbushana na kupeana mikakati ya kujiondolea umaskini sisi wenyewe, basi kamwe hakuna mtu wa kuja kutuondolea" alisema.
Amesisitiza Wanawake kuungana na kuweza kufanya harakati za kujikomboa na umaskini pamoja. Hili ni tukio la pili kuandaliwa na kikundi cha umoja wa wanawake Tanga (Wochata) baada ya awali kuandaa event kama hiyo tarehe 3 mei  mwaka huu. Katika shughuli hiyo Wochata waliwaalika watoa mada Regina Mwaleka (mada ya ndoa) na Joy Nyambogo (mada ya Ujasiriamali). Mgeni rasmi katika shughuli hiyo alikuwa Madam Latifa Shehoza.


Mgeni rasmi, Madam Latifa Shehoza (katikati) akiwa na Mtangazaji maarufu Regina Mwaleka (Kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Wochata Risala A. Samiji katika Shughuli ya Wochata iliyofanyika mwezi mei 3, 2014.