Mwanadada Mc mahiri,
Miriam Migomba amezungumzia tukio la
wochata jol kuwa litaweka historia na kubadilisha maisha ya wanawake wa Tanga. Akiongea kwa njia ya simu na blogu hii amesema amejiandaa vya kutosha kuja kutoa somo kwa watakaoshiriki siku hiyo.
Mwanadada Miriam Migomba
"Nachoweza kusema wanawake wenzangu wa Tanga, watambue kuwa kama hatuna desturi ya kukumbushana na kupeana mikakati ya kujiondolea umaskini sisi wenyewe, basi kamwe hakuna mtu wa kuja kutuondolea" alisema.
Amesisitiza Wanawake kuungana na kuweza kufanya harakati za kujikomboa na umaskini pamoja. Hili ni tukio la pili kuandaliwa na kikundi cha umoja wa wanawake Tanga
(Wochata) baada ya awali kuandaa event kama hiyo tarehe 3 mei mwaka huu. Katika shughuli hiyo Wochata waliwaalika watoa mada
Regina Mwaleka (mada ya ndoa) na
Joy Nyambogo (mada ya Ujasiriamali). Mgeni rasmi katika shughuli hiyo alikuwa
Madam Latifa Shehoza.
Mgeni rasmi, Madam Latifa Shehoza (katikati) akiwa na Mtangazaji maarufu Regina Mwaleka (Kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Wochata Risala A. Samiji katika Shughuli ya Wochata iliyofanyika mwezi mei 3, 2014.